Habari mpya

Mh. Mwigulu Nchemba awataka waliosababisha maafa kukamatwa mara moja na kupelekwa kunakohusika

 
Kufuatia migogoro ya ardhi inayoendelea sehemu mbalimbali hapa nchini hasa baina ya wafugaji na wakulima na ile ya wananchi na wawekezaji imemlazimu Mh. Mwigulu Nchemba kufika Mkoani Morogoro wilaya ya Mvomero ambako yalitokea maafa kufuatia vurugu baina ya wakulima na wafugaji. Nchemba amelaani vikali maafa hayo na kutoa rai ya wahusika waliotekeleza unyama huo kukamatwa mara moja na kufikishwa mahakani na kuwaasa wananchi kuacha kujichukulia hatua mkonini.
Pia amesema zitaundwa kamati kwa kila kijiji kwa pande zote mbili ilizoingia katika mgogoro ili kubaini ni nani hasa mvamizi wa eneo la mwenzakeili hatua iweze chukua mkondo wake.
Pia amemuagiza mkuu wa wilaya ya Mvemoro kuhakikisha watu waliojeruhiwa, wanapatiwa matibabu kwanza bila kuchelewa na hatua za kisheria kwa wenye hatia zifuate.
Endela kufuatilia Mwanaharakati Mzalendo Media kwa taarifa zaidi.

No comments