MTAZAMO WA RAMA DEE KUHUSIANA NA ZITTO KABWE KUVULIWA MADARAKA KATIKA CHAMA CHA CHADEMA
Nimekaa na kutafakari nimegundua mambo mengi sana katika Nchi yangu 
yenye Watu wenye matumaini....matatizo ya Chama cha Chadema ni sawa na 
matatizo ya NCCR na CUF miaka iliyopita,Chama cha NCCR kilipewa 
matumaini makubwa  na Wananchi miaka ya tisini kikiongozwa na mwenyekiti
 wake Mrema lakini zilifanyika mbinu kubwa za kukipunguza nguvu chama 
hiki na si vingine kuwatumia watu ambao wapo ndani ya chama wenye nafasi
 za juu...chama hiki walifanikiwa kukilipunguza nguvu na Wananchi 
walipoteza imani kabisa, lakini inafikia sehemu Wananchi Haswa Wasanii 
wenzangu tunatakiwa kusimama na Kutoziamini hizi propaganda pia inafikia
 wakati wa kila mwananchi kufahamu mipango ya chama kama chama, Chadema 
kumvua vyeo bwana Zitto ni sahihi kwa maslahi ya chama na katiba ya 
chama hilo sio la kujadili,  tujadili je hii njia ambayo inatumiwa na 
Chama tawala kuvunja upinzani je tunaikabili vipi maaana inajirudia tu 
kila ikifika uchaguzi mkuu wanatengeneza njia za kuvuruga
 utaratibu, naomba tusiamini haya ambayo yapo mbele yetu tuamini kile 
chama ambavyo kinasema nafikiri ndio njia rahisi ya ukombozi wa 
elimu,afya nk,matatizo ya zitto haya tuhusu kwa sababu amevunja 
utaratibu (kanuni) na chama kimethibitisha, Mbowe ni mwana chama na 
kiongozi angekuwa anania mbaya na zitto basi hata hizo fulsa ambazo 
amepata zitto asingezipata, mwanzo sikumfahamu ZITTO nilikifahamu Chama 
na Chama kilimtambulisha, tukumbuke kila Chama kinaongozwa na katiba na 
ndio maana ya Chama... Watanzania  tumebakiza muda kidogo sana kupata 
mabadiliko ni sisi kusimama na kuangalia wapi tunaelekea hizo ni siraha 
za chama tawala kwenye kukimaliza chama na naaamini hawawezi MUNGU 
BARIKI CHADEMA NA VIONGOZI WAKE yesu alisalitiwa kwenye Movment 
zake,lakini aliendelea mbele mpaka walipoona wamemshindwa walimmaliza 
ila ukweli ulibaki na upo mpala leo.... WATANZANIA TUSIMAME VIONGOZI 
WANAFANYA AKILI ZETU KAMA "PLAY STATION TUSIMAME JAMANI HASWA VIJANA 
WENZANGU NA WANAFUZI WA VYUO asanteni. USISHANGAE LEO KUONA ZITTO YUPO 
CCM!!!!!
Source: Facebook (Rama Dee) 

No comments